Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

YALIYONIKUTA SITAKI YAKUKUTE WEWE, EBU JIFUNZE KUPITIA HAPA

Kwa wale watu kwa ujumla wanaoingia Kwenye Mahusiano hasa ya kudumu, yanaweza Kuwa ndoa au ya mwelekeo wa ndoa ni vyema tukawa tumejiandaa kwa lolote litakalotokea na kulichukulia hata kama ni nzito namna gani.

Kumbuka hakuna kitu kisichokuwa na mapito au changamoto kosa kubwa tunalolifanya pale tunapoingia kwenye mahusiano hayo ni pale tunapofikiri kuwa mwenzi wako huyo ni malaika na hawezi kukosea kwa namna yoyote ila Wewe ndio binadamu ukikosea usamehewe na muendelee kuvumiliana ila wewe uvumilivu huna.


Pale mnapompenda mtu jua kuwa na yeye anamadhaifu yake ambayo unatakiwa kumvumilia hata kama ni ya namna gani, hata iwe ni usaliti wa ndoa ni lazima mvumilie na sio kumuacha au kumkashifu.Utakuta mtu anasema kwa jambo hili siwezi vumilia na anasahau hata yeye anavumiliwa tu.

Ni lazima tujue kuwa huwa tunakutana na watu wanaotufaa kwa yale Madhaifu Yetu na sio watu wakamilifu wa madhaifu yetu, yaani mfano unaweza kukuta mwanamke hawezi labda kufua nguo vizuri na wewe swala la kufua nguo sio shida sana.

So unachotakiwa kufanya sio kudharirisha na kuwa na akili mgando ya mfumo dume hapo ni kuweka mfanya kazi au fua na sio kudharirishwa kwani mke sio mfanyakazi na kuna tofauti ya majukumu ya mfanyakazi na mke pia na heshima zao zinatofautiana, au mwanaume ni bwana mipango mzuri lakini utekelezaji wako ni ziro nawe unaweza kusimamia. Hivyo we simamia na usiwe na dharau, kwani sifa ya kwanza ya mwanamke ni utii.



This post first appeared on Mutalemwa, please read the originial post: here

Share the post

YALIYONIKUTA SITAKI YAKUKUTE WEWE, EBU JIFUNZE KUPITIA HAPA

×

Subscribe to Mutalemwa

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×